Kituo hicho kimeweza kuinua kipata cha mabinti waliokuwa hawajiwezi na wengine kutaka kujiua. Moja ya mambo yanayofanyika katika kituo hocho ni kujifunza ushonaji na ufumaji. Pia mama huyo ameweza kuwasaidia jamii ya wamang’ati kwa kuwaanzishia mrati wa kufuga mbuzi na nyuki wa asali. Pamoja na kituo hicho, pia anacho kituo cha kulea watoto yatima.

Inawezekana wewe ni Binti, umezalishwa na kutelekezwa, au unaye binti wa aina hiyo, au ungependa kuwa rafiki wa maono haya ya Bi Lightness, kwa kumuombea, kumtia moyo au kuchangia chochote, basi usisite kuwasiliana naye kwa simu namba 0754317394
John Shabani katika kijiji cha Mang'ola huko karatu
Bi Lightness akimuonyesha John shughuli mbalimbali zinazofanywa na chuo cha Lake Eyesi Vocation Training Center
0 comments:
Post a Comment