Friday 18 April 2014

Tasisi ya kusaidia vijana, na jamii mbalimbali kuanzishwa

Baada ya kuzunguka nchi kadhaa barani Afrika na kujionea hali ngumu ya maisha ya watu hasa kina mama watoto na vijana, John Shabani yuko mbioni kukamilisha usajili wa taasisi yake ijulikanayokama HOPE TRUST, yenye lengo la kutafuta ufumbuzi katika kuwasaidia watoto, kina mama, vijana  na wote waishio katika mazingira magumu

Taasisi hiyo itajikita katika kutafuta ufumbuzi katika kuwasaidia watoto, vijana na kina mama wanaoishi katika mazingira magumu. Hivi karibuni John alifanya ziara huko Turkana Kenya maali ambapo kuna jamii ya watu wanaoishi katika mazingira magumu sana na walioshikilia mila na tamaduni zilizo kinyume na haki za binadamu, pia alitembelea katika moja ya kambi kubwa ya wakimbizi barani Afrika; kambi hiyo inaitwa KAKUMA, yenye wakimbizi kutoka Uganda, Rwanda, DRC Kongo, Burundi, Somalia, Rwanda n.k.
Pia John alitembelea vijiji kadhaa huko Sudan, na kujionea jinsi maisha yalivyo magumu hasa kutokana na vita vya mara kwa mara katika nchi hiyo amba yo hivi karibuni imegawanyika na kuwa nchi mbili.

Kwa upande wa Tanzania, John amekuwa akifanya ziara mbalimbali, akitembelea jamii ya watu wanaoishi katika mazingira magumu na hasa wale waliokumbatia mila zinazorudisha nyuma maendeleo. Katika ya makabila hayo ni wa Hadzabe, wa Mang’ati, wa Masai na makabila mengine madogomadogo.

Kwa msaada wa Mungu, John amepanga kutembelea huko Somali, Kongo, Misri na nchi zingine barani Afrika.
Pia ili kuibua vipaji kwa vijana na watoto na kuviendeleza, ameanzisha kituo cha kuibua vipaji, na kwa kuanza, ameanzisha kituo cha kuibua vipaji vya uimbaji na uigizaji. Mpaka sasa kituo hicho kimeibua vipaji vya watoto 35, vijana 105 na watu wazima 22.

Unapoomba, usisahau kulitaja jina la John Shabani, mwana harakati aliyejitolea kwa nguvu zake, Vipaji vyake pamoja na uwezo wake mdogo kuwasaidia watu wengine.

Watu hawa wanahitaji msaada wa kila aina ili waweze kuishi kama mwanadamu mwingine.

Wito wangu, ni kwa kila mtu kuguswa na na hali hii na kuungana namikatika kuwasaidia ndugu zetu hawa. Usiulize serikali imekufanyia nini, bali jiulize umechangia nini katika serikali yako. Kumbuka amsaidiaye maskini humkopesha Mungu, na Mungu wetu hawezikukaa na deni la mtu,yeye hulipa mara mia. Ukitaka kujua maisha magumu, tembelea vijijini. Kumbuka mchango wako wa hali na mali ni wa muhimu sana. Mchango wako na wangu hakika unaweza kuwasaidia ndugu zetu hawa.

0 comments:

Post a Comment